Jumamosi , 4th Jun , 2022

Waziri wa Maliasili Dkt. Pindi Chana, amesema serikali imesaini mkataba wa ushirikiano katika masualan ya utalii, biashara na uwekezaji baina ya Tanzania na Jiji la Dallas Marekani, hatua itakayowezesha safari za moja kwa moja za ndege kutoka Tanzania hadi Dallas, Marekani.

Air Tanzania

 

Waziri Dkt. Chana amesema uwepo wa safari za ndege za Tanzania za moja kwa moja hadi Dallas nchini Marekani zitasaidia kuongeza idadi ya wageni wataokuja nchini kutembelea hifadhi na ameneo yote ya utalii, haya yakiwa ni matokeo chanya ya filamu ya Royal Tour.

Aidha hapo jana wakati wa mawasilisho ya makadirio ya bajeti ya Wizara ya Maliasili bungeni Dodoma, baadhi ya wabunge waliishauri serikali kuongeza kasi ya kutatua changamoto ya migongano kati ya binadamu na wanyamapori ambayo inahusisha Hifadhi na makazi ya wananchi.