Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

RC Malima aapa kupambana Mwekezaji apate leseni

Ijumaa , 13th Mei , 2022

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima amesema serikali ya mkoa kwa kushirikiana na Serikali Kuu, Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara  watafanya kila linalowezekana ili mwekezaji wa Kiwanda cha kuzalisha vilainishi na mafuta kwa ajili ya mashine na magari cha Mogas, kilichopo jijini Tanga

RC Malima ameyasema hayo wakati alipotembelea kiwanda hicho mara baada ya kupata malalamiko ya kukwamishwa kwa mwekezaji huyo katika upatikanaji wa leseni.

“Nataka nimhakikishie mwekezaji Mogas serikali itafanya kila linalowezekana ili apate leseni na kila anachohitaji kifanyike ili uwekezaji uende mara mbili. Sasa hao wanaokuja wanatoa taswira kwa watu wengine kwamba Tanga ipo kwa ajili yakupokea mitaji na uwekezaji na wanapeleka ujumbe mzuri kwa watu wengine na serikali ya mkoa tunawaunga mkono kwa asilimia 100" 

“Katika Mkoa wa Tanga nimeweka utaratibu wa kuhamasisha wawekezaji kushiriki na sisi moja kwa moja kwenye maendeleo ya serikali ya mkoa, kwa hiyo kama kuna mwekezaji amekuja ana jambo lake urasimu umekuwa mwingi tunataka kuviondoa hivyo"

“Leo kuna mwekezaji amekuja kufuatilia upatikanaji wa vibali akaambiwa asubiri miezi sita na sasa umepita mwezi mmoja na nusu, leo kaja kuniambia Mheshimiwa hatutaki kuwachongea lakini miezi sita kweli, na hicho kibali chenyewe mimi nauliza ni cha kusaini kwa mkono sasa kusaini kwa mkono miezi sita"

“Kwa hiyo sasa hawa wenye matendo ambayo mimi nawaita ya kipuuzi kumzuia mwekezaji ambaye amekuja nchini kwako kwa lengo la kuleta mitaji na mambo mengine, uwekezaji ule ndiyo unaleta ajira za ziada na kodi hata mzunguko wa fedha,” amesema RC Malima. 

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mogas, Geofrey Rugazoora alisema wanaishukuru serikali mkoani Tanga ambapo pia ameahidi kutoa mchango chanya katika kuchangia maendeleo mkoani hapa.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu