Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan.
Akitoa maelezo kwa Rais Samia katika maonesho ya kilele cha sherehe ya wakulima Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema kila kisima kitakuwa na uwezo wa kuhudumia wakulima 16.
Amesema kisima hicho kitakuwa na tenki la lita 5000 litakalokuwa limefungwa mfumo wa umeme jua (sola panel) kwa ajili ya ku-pump.
"Pia mkulima atapewa eneo la umwagiliaji la heka 2.5 na mkulima wa kwanza katika program hii anatoka wilayani Mbarali mkoani Mbeya," amesema.
Aidha, akizungumzia mradi huo, Rais Samia amempongeza Bashe kwenye eneo hilo umwagiliaji maji kwa kufanikiwa kutumia vyanzo mbalimbali ikiwamo skimu za umwagiliaji.