
Rais Samia akiwa kwenye Soko la Nzega Parking
Rais Dkt. Samia ametoa fedha hizo alipotembelea soko hilo kufuatia ombi la Mbunge wa Nzega na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe kumuomba kutembelea soko hilo ambapo mbali na ujenzi wa soko lakini pia ametoa mitaji kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wa soko hilo.
Aidha Rais Dkt. Samia amewataka wafanyabiashara hao kupisha ujenzi na kuwaelekeza Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kuhakikisha soko likikamilika wafanyabiashara waliopisha ujenzi ndio wapewe kipaumbele.