Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Prof afikishwa mahakamani baada ya kuoa kwa siri

Jumanne , 24th Jan , 2023

Mahakama ya wilaya ya Morogoro imempandisha kizimbani Profesa Christopher Kasanga wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa shtaka la ugoni baada ya kufunga ndoa ya pili kwa siri na mwanamke mwingine Oktoba 29 mwaka 2022

Profesa Christopher Kasanga, akiwa na mke wake aliyemuoa kwa siri

Imeelezwa kuwa kesi hiyo ya madai namba 57/2022 imefunguliwa Desemba 16, 2022 na Matlida Sigareti dhidi ya mumewe Profesa Christopher Kasanga ambaye wamefunga ndoa miaka 25 iliyopita.

Bi. Matlida amelazimika kufungua keshi hiyo baada ya kubaini mume wake Profesa Kasanga kufunga ndoa nyingine kwa siri na mwanamke mwingine anayefahamika kwa jina la Linael Makundi ambaye ni mfanyakazi wa Benki ya CRDB.Mjini Morogoro.

Kesi hiyo inasikilizwa chini ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Morogoro Emmael Lukumai, ambapo katika upande wa mashtaka kesi hiyo inasimamiwa na wakili Emmanuel Chengula na Gervas Semgabo wakati upande wa utetezi ikisimamiwa na wakili Asifiwe Alinanuswe.

Akizungumza nje ya mahakama hiyo Wakili wa mlalamikaji Emmanuel Chengula amesema kesi hiyo imesikilizwa kwa mara ya kwanza mbele ya Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo ambapo mteja wake ambaye ni Matlida Sigareti anadai kulipwa fidia ya shilingi milioni 100 za Kitanzania kutokana na madhara ambayo ameyapata.

Kwa upande wake Wakili wa utetezi Asifiwe Alinanuswe alipotakiwa kuzungumzia shtaka hilo alisema hajapewa maelekezo ya kuzungumzia kesi hiyo kutoka kwa mteja wake.

Hata hivyo, Hakimu Mfawidhi Lukumai ameahirisha kesi hiyo baada ya upande wa utetetezi kuweka pingamizi la kutaka kesi hiyo isikilizwe faragha ambapo imepangwa kusikilizwa tena Februari 21 mwaka huu.

HABARI ZAIDI

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea

Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri, CDF Mpya wa Kenya

Luteni Charles Muriu ateuliwa kuwa CDF mpya Kenya