Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Odinga ajiondoa kugombea urais Kenya

Jumanne , 10th Oct , 2017

Mgombea Urais kupitia muunganiko wa vyama vya upinzani nchini Kenya, Raila Amolo Odinga, amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho, baada ya viongozi wa Tume ya Uchaguzi Kenya IEBC, kukataa kuachia madaraka.

Akiongea na vyombo vya habari jijini Nairobi Kenya, kiongozi huyo wa upinzani ameituhumu Tume inayosimamia uchaguzi nchini humo IEBC kwa kutotaka kubadili uongozi wake, ambao wanaamini unampendelea Uhuru Kenyatta.

“Kwenye katiba ya demokrasia, hatukutakiwa kubishana kuhusu uchaguzi huru na haki, tulitakiwa kufanya kazi kwa pamoja kuhakikisha tunasimamia uchaguzi huu na mfumo wake wa kielektoniki, lakini kuendelea na uchaguzi bila marekebisho kwenye IEBC ni misingi ya vikwazo kwa huu uchaguzi, uchaguzi pekee ambao Jubilee wanataka ni ule ambao lazima watashinda hata kama sio kwa sheria”, amesema Raila Odinga.

Uamuzi huo wa Raila Odinga umekuja siku moja baada ya Uhuru Kenyatta kumtaka ajitoe kwenye kinyang'anyiro kama hayuko tayari kurudia uchaguzi huo ulioamriwa na mahakama.

Pamoja na hayo viongozi hao wa NASA wameitisha maandamano ya nchi nzima hapo kesho asubuhi, ili kupinga kitendo cha Tume ya Uchaguzi kutobadili uongozi wake.

Septemba 1, 2017 Mahakama ya Juu nchini Kenya ilfuta matokeo ya uchaguzi wa Urais baada ya NASA kuishtaki IEBC kwamba walifanya udanganyifu na kukutwa na hatia, na kuamuru uchaguzi huo urudiwe ndani ya siku 60, ndipo Tume ya Uchaguzi ikaitangaza Oktoba 26 kuwa siku ya uchaguzi wa Urais.
 

 

 

 

Endelea kubaki nasi kwa taarifa zaidi.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu