Jumamosi , 4th Dec , 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amemtaka Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, afanye marekebesho yanayowezekana ndani ya wizara yake ili mambo yaendelee kufuatia uwepo wa ubadhirifu mkubwa katika bandari ya Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, na kulia ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa

Kauli hiyo ameitoa hii leo Desemba 4, 2021, jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa gati 0 hadi 7 ya Bandari ya Dar es Salaam.

"Mh. Waziri nilikuweka kwa kukuamini na ninaomba nenda kasimamie kazi hii kama ninavyotarajia na utakaposhindwa njoo uniambie, Dada nimeshindwa, nitaangalia mwingine labda ataweza kunisaidia, lakini haya hayawezi kuendelea," amesema Rais Samia.