
Mh. Zambi amefikia hatua hiyo baada ya aina hiyo mpya ya kodi kuja na viwango vikubwa, ambavyo pia vimekuja kipindi ambacho kiuchumi wakulima wengi hawawezi kuimudu kwa kuwa bado mavuno hayajaanza.
Kwa upande wao wakulima katika wilaya hiyo ya Mbozi wamependekeza serikali kuachana na bima ya moto na badala yake kuelekeza bima hizo kwenye mashamba ya kahawa, hasa kwenye majanga ya asili kama mvua za mawe, ambazo zimekuwa zikiwatia hasara wakulima kwa baadhi ya misimu.