Jumamosi , 19th Apr , 2014

Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amewataka Watanzania kuhakikisha wanadumisha na kuulinda Muungano ili kizazi kijacho kiweze kuyaona mafanikio na changamoto za shughuli hizo tangu kuanzishwa kwa Muungano.

Rais Mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi

Rais Mstaafu alitoa kauli hiyo jana alipotembelea mabanda nane ya sekta mbali mbali zinazohusika na masuala ya Muungano na kuoneshwa mafanikio na changamoto za shughulii hizo tangu kuanzishwa kwa Muungano.

Mzee Mwinyi alisema kuna baadhi ya Ofisi na Tume ambazo alikuwa hajui zinafanya kazi gani tangu kuanzishwa kwa Muungano, na kuwa fursa kwake kuona mafanikio ya Muungano kupitia sekta alizozitembelea