Jumanne , 13th Aug , 2024

Mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa bongo fleva Joseph Francis Michael maarufu kama Mandojo umewasili nyumbani kwao wilayani Manyoni mkoani Singida jioni ya leo Agosti 13, 2024, ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho Jumatano katika makaburi ya Kaloleni Manyoni.

Jeneza lenye mwili wa Mandojo

Mandojo alifariki siku ya Jumapili Agosti 11 mkoani Dodoma baada ya kupigwa katika moja ya kanisa ambapo hadi sasa Jeshi la Polisi linamshikilia mlinzi wa kanisa hilo kwa uchunguzi zaidi.