
Kamanda wa Polisi Mkoa wa mwanza, Ahmed Msangi
Tukio hilo limetokea katika mtaa wa Medical Kata ya Kitangiri ilemela jijini Mwanza na mwili wa kichanga hicho umegunduliwa na watoto baada ya kuona kichwa kikiwa nje ya mfuko aina ya lambo damu zikitoka.
Mwenyekiti wa Mtaa huo Bw Patrober Maginga akiwa eneo la tukio amelaani kitendo hicho cha kikatili na kwamba uongozi wa mtaa kwa kushirikiana wananchi watafanya uchunguzi kumbaini mhusika wa tukio hilo na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria.
Aidha Jeshi la Polisi kituo cha Kirumba Jijini humo wamefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa kichanga hicho kwa uchunguzi na hatua zaidi.