
Habari za kupatikana kwa mwili huo zimethibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei ambaye amesema mwili huo ni wa mtoto mdogo na kufafanua kuwa ajali hiyo ni ya Mtumbwi kugongana na Pantoni inayotoa huduma katika mto huo.
Kamanda Matei amefafanua kuwa katika ajali hiyo watu wanane walizama katika mto Rufiji na kwamba jitihada za kuwatafuta watu wengine saba wanaohofiwa kufa maji zinaendelea.