Ijumaa , 13th Aug , 2021

Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Makampuni ya ASAS, Alhaj Faraj Ahmed Abri, amefariki dunia hii leo Agosti 13, 2021 Jijini Dar es Salaam, na familia yake imeomba waombolezaji wasiende nyumbani na atazikwa hii leo katika Makaburi ya Kisutu.

Mwanzilishi na Mwenyekiti wa Makampuni ya ASAS, Alhaj Faraj Ahmed Abri

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya familia ya ASAS imeleza kwamba, njia ya teknolojia za habari itumike katika kutoa pole na shughuli zingine za msiba na si kukusanyika nyumbani.