Picha si halisi
Mwanamke huyo aliyefahamika kwa jina la Mbonamengi Mabayi, alitengwa na jamii baada ya kugoma kuhudhuria kwenye msiba wa jirani yake aliyefariki kwa kujinyonga.
Mbunge wa jimbo la Geita Vijijini, Joseph Kasheku (Musukuma) akataka ufafanuzi wa jambo hilo kutoka kwa viongozi ambapo Mwenyekiti wa Kitongoji cha Chabwa Maganga Kaboya akabainisha sababu ya Mwanamke huyo kutengwa na wanakijiji wenzake, na kumueleza Mbunge huyo kuwa suala hilo kwa sasa lipo mahakamani.

