Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mvua yaua watu wawili, yajeruhi 26 kanisani

Jumatatu , 20th Feb , 2017

Watu wawili wamefariki dunia wakiwa kanisani katika ajali ya mvua iliyokuwa na upepo mkali huku wengine 26 wakijeruhiwa, wilayani Magu mkoani Mwanza.

Picha: Maktaba

Tukio hilo limetokea jana jioni katika Kijiji cha Lubungu, wilayani Magu mkoani Mwanza ambapo watu hao wametambulika kwa majina ya Ngwaku Nkulumbi (55) ambaye ni mwanamke na mtoto wa kike  Migayi Herenico (12)

Taarifa ya Jeshi la Polisi mkoani humo imeeleza kuwa tukio hilo limetokea baada ya upepo mkali kuezua paa la kanisa la dhehebu la Roman Catholic wakati waumini wa kanisa hilo wakiendelea na ibada.

Taarifa hiyo imesema kuwa , kati ya majeruhi hao 26, majeruhi 7 hali zao bado siyo nzuri wamepelekwa hospitali ya rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi huku majeruhi 17 wakiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya wilaya ya magu na majeruhi 02 tayari wameruhusiwa.

Ahmad msangi - RPC mwanza

Jinsi ilivyokuwa.....

Inasemekana kuwa ibada hiyo ilikuwa imehudhuriwa na zaidi ya waumini 100, lakini ilichelewa kuanza kwa sababu Padre wa Kanisa hilo aitwaye Michael Kumalija miaka 60 ambaye  alikuwa ameanza kuhudumia katika kanisa la jirani alichelewa kufika kanisani hapo.

Padre huyo alifika majira ya saa 9 Alasiri, na dakika chache baada ya ibada kuanza, mvua kubwa iliyoambatana na upepo ilianza kunyesha.

Aidha inadaiwa kuwa baada ya tukio hilo kutokea waumini walianza kukimbia kutoka nje ya kanisa huku kila mmoja akijaribu kunusuru maisha yake, ndipo baada ya tukio hilo kupita iligundulika kuwa watu wawili wamefariki dunia

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali