Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mollel, Waitara, Silinde waneemeka CCM

Alhamisi , 29th Oct , 2020

Katika uchaguzi huu Chama Cha Mapinduzi (CCM) miongoni mwa wagombea wake wa ubunge nchi nzima pia walikuwemo wagombea watatu  wa ubunge ambao walitokea Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika miaka ya mwanzoni na wengine dakika za lala salama bunge likiwa linaelekea kuvunjwa,

Pichani ni Wabunge wateule kwa tiketi ya CCM, Kushoto ni Godwin Mollel (Siha), Mwita Waitara (Tarime Vijijini), Kulia ni David Silinde (Tunduma)

 kuvunjwa ambao ni Mwita Waitara, Godwin Mollel na David Silinde.

Kwa upande wake David Silinde hapo awali alikuwa Mbunge wa jimbo la Mbozi Mjini tangu 2010  kwa tiketi ya CHADEMA baada ya kuhamia CCM na kupitishwa kuwania ubunge aligombea jimbo la Tunduma ambapo ameibuka msindi kwa kura 43,276 dhidi ya mshindani wake Frank Mwakajoka wa CHADEMA aliyepata kura 12,433.

Aidha kwa upande wa Dkt Godwin Mollel yeye aliingia Bungeni mwaka 2015 na mwaka 2017 alikihama chama chake ''CHADEMA'' na kutimkia CCM, Disemba 2017 akiwa sehemu ya kuunga mkono juhudi zilizokuwa zikifanywa na serikali ya awamu ya tano, katika uchaguzi mdogo uliofanyika Februari 2008 Mollel aliibuka mshindi kwa kupata kura  25,611 huku Elvis Mosi wa CHADEMA akipata kura 5,905 na katika uchaguzi Mkuu huu amepata kura 22,172, akifuatiwa na Elvis Mossi wa CHADEMA aliyepata kura 8614.

Kwa upande wake Mwita Waitara alichaguliwa kuliongoza Jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CHADEMA mwaka 2015, alijiuzulu na kujiunga na CCM mwezi Julai 2018 na baada ya siku 4 tangu kuapishwa kwake bungeni Waitara aliteuliwa na Rais John Magufuli  tarehe 10 Novemba 2018 kuwa Naibu waziri wa TAMISEMI katika mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali