Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkurugenzi adaiwa kuuza viwanja vya serikali

Ijumaa , 27th Jan , 2023

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Adam Malima, amepokea ripoti ya uchunguzi kuhusu tuhuma za kuuza viwanja vya serikali vinavyodaiwa kuuzwa shilingi bilioni 1 kinyume na taratibu na Mkurugenzi wa jiji hilo Selemani Sekiete, vilivyopo Halmashauri ya wilaya ya Nyamagana mkoani humo.

Selemani Sekiete, Mkurugenzi wa jiji la Mwanza

Akipokea ripoti hiyo, mkuu huyo wa Mwanza Adam Malima amesema kamati hiyo ya maadili imefanya kazi kubwa katika kufuatilia suala hilo na kuahidi kufanyia kazi yote yaliyoelezwa na kamati hiyo.

Aidha RC malima ameagiza kufuatilia migogoro yote ya ardhi katika mkoa huo kwani imekuwa tatizo linalojirudia kila mara kutokana na malalamiko ya wananchi anayopokea.

"Inaonekana kumekuwa unyang’anyi wa viwanja ndani ya Mwanza, kwamba mtu una kiwanja chako anakuja mtu mjanja kupitia idara ya ardhi na watendaji wake unanyang'anywa kiwanja chako its not fair na mara nyingi watu wanofanyiwa hivi ni watanzania wa hali ya chini na huenda ardhi ile ingekuwa ni jambo la manufaa kwake," amesema RC Malima

Awali akikabidhi ripoti hiyo Mkurugenzi wa Tume ya Maadili ya Viongozi kanda ya Ziwa Godson Kweka, amesema wakati wakikamilisha uchunguzi huo walibaini matatizo mengine ya ardhi na hivyo kuomba kuongezewa muda wa kufanya uchunguzi zaidi.

Kamati hiyo imetumia siku nane kuchunguza kuhusu uuzwaji wa viwanja viwili vya serikali namba 194 na 195 vinavyodaiwa kuuzwa kwa shilingi bilioni 1 na kupelekea hivi karibuni mkuu wa mkoa huo wa Mwanza Adam Malima kumshtaki kwa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji hilo Selemani Sekiete kwa kuuza viwanja hivyo huku watumishi wengine wanne wakisimamishwa kazi kupisha uchunguzi wa uuzwaji wa viwanja hivyo.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA