Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mkiniona naharibu alaumiwe Makinda- Spika Ndugai

Ijumaa , 11th Jun , 2021

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema kuwa endapo ikitokea ameharibu katika kazi zake basi wa kulaumiwa ni Spika Mstaafu wa Bunge Mama Anne Makinda, kwani yeye ndiye aliyekuwa akimwongoza tangu awali.

Kushoto ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, na kulia ni Spika wa Bunge Mstaafu Mama Anne Makinda

Kauli hiyo ameitoa Bungeni Dodoma, jana jioni Juni 10, 2021, wakati akimkaribisha Bungeni, na kuongeza kuwa Mama Makinda, amekuwa ni mwalimu wake kwa kipindi kirefu tangu alipoingia Bungeni kwa mara ya kwanza.

"Mama Makinda amekaa humu Bungeni takribani miaka 40 hii rekodi siyo rahisi na yeye alikuja kama mbunge kijana, nilipoingia hapa Bungeni nilipangwa kwenye Kamati ya Ardhi Maliasili na Mazingira na yeye akawa ni Mwenyekiti wangu, miaka mitano iliyofuata yeye akawa Mwenyekiti wa Bunge mimi akaniachia kijiti kwenye kamati," amesema Spika Ndugai.

"Baadaye akawa Naibu Spika mimi nikawa Mwenyekiti wa Bunge yeye akawa Spika wa Bunge mimi nikawa Naibu Spika, ameenda kustaafu nimekuwa Spika kwa hiyo mimi huwa nafuata mguu wake anapotoa mimi naweka sasa kwa vile alishastaafu na mimi nafuatia nitakuja kuwaambia huko mbele, namshukuru sana Mama kwa malezi mkiniona naharibu alaumiwe yeye maana yeye ndiyo mwalimu wangu kila hatua," ameongeza Spika Ndugai.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu