Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mitumbwi inavyotumika kuvusha watu

Ijumaa , 14th Mei , 2021

Wakazi wa kata tatu za Katoro, Kyamulaile na Ruhunga zilizoko katika halmashauri ya wilaya ya Bukoba mkoani Kagera wameiomba serikali kuwaondolea kero ya kuvuka kwa mitumbwi katika eneo la Katokoro, iliyosababishwa na barabara yao kuvunjika na kujaa maji, tangu msimu wa mvua 2019.

Wakazi mbalimbali wakiwa kwenye kivuko

Wakizungumzia kero hiyo wakazi hao wamesema kuwa ni takriban miaka mitatu sasa wanateseka na kwamba tatizo hilo limesababisha gharama za usafiri na usafirishaji kupanda.

Mmoja wa wananchi hao Imani Abeid mkazi wa kijiji Katokoro amesema kuwa zamani walitumia shilingi 1,000 kutoka kijiji hicho kwenda Katoro na kurudi, lakini kwa sasa wanatumia shilingi 6,000 kwenda na kurudi.

"Ukitoka hapa Katokoro kwenda Katoro utapanda bodaboda ulipe shilingi 1,000 na pia utalipa shilingi 1,000 ili uvushwe kwa mtumbwi, ukishavuka kwa kuwa hata upande wa pili hakuna magari utapanda tena bodaboda hadi Katoro kwa kulipa shilingi 1,000 hapo jumla ni shilingi 3,000 ambayo kwenda na kurudi ni shilingi 6,000" amesema Abeid.

Akitoa ufafanuzi kuhusiana na changamoto hiyo meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini - TARURA- katika halmashauri ya wilaya hiyo mhandisi Ally Maziku amesema kuwa serikali imeanza kulifanyia kazi suala hilo, na kuwataka wananchi kuwa na subira.

"Mkandarasi aitwaye Rumanyika alikuwa tayari kazini, kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha amesitisha kazi kwa muda, lakini nina imani kufikia Septemba mwaka huu kazi ya kutengeneza barabara katika eneo hilo itakamilika kwa mujibu wa mkataba" amesema mhandisi Maziku.

Kwa upande wake mratibu wa TARURA Mkoa wa Kagera mhandisi Avity Theodory amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto za ubovu wa barabara katika maeneo korofi wanalazimika kuomba fedha nje ya bajeti.

"Bajeti ya Tarura mkoa ni shilingi bilioni 9.3,  tumeomba fedha nje ya bajeti hiyo tukapata shilingi milioni 485 kwa ajili ya kutengeneza eneo hilo la Katokoro, lkn pia tumepata shilingi milioni 80 kwa ajili ya matengenezo ya barabara eneo la Rwabwere Karagwe" amesema mhandisi Theodory.

Jumla ya mitumbwi 33 inatumika kuvusha wananchi katika eneo hilo la Katokoro.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali