Jumamosi , 5th Dec , 2015

Serikali ya Tanzania imeziomba nchi za Jumuia ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika SADC kuhakikisha zinakuwa na mfumo wa kuangalia matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ili isiendelee kusababisha madhara katika jamii.

Mkurugenzi wa Idara y Habari MAELEZO Assah Mwambene ametoa kauli hiyo jijini Dar es salaam wakati akifungua mkutano wa 10 uliwaoshirikisha wadau wa utangazaji kwa njia ya Digitali kutoka nchi za SADC.

Mwambene amesema mitandao hiyo ya kijamii imekuwa ikisababisha kuporomoka kwa madili na hivyo kuharibu na jamii ambayo imekuwa ikitumia mitandano hiyo kwa njia zisizo halali na kujifunza mambo mbayo huchangia kuharibu tabia.

Mwambene amesema mitandao ya kijamii inatumiwa vibaya na hivyo kuhatarisha amani na usalama wa nchi na wanainch wake