Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza James Ruge
Akitoa taarifa hiyo Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mwanza James Ruge, amesema ufuatiliaji ulifanyika katika miradi 35 mkoani humo katika sekta za afya, barabara, elimu na utawala ambapo mapungufu katika miradi hiyo 27 yalikuwa ni kujengwa chini ya kiwango, uchepuzi wa vifaa na kutumia vifaa duni visivyokidhi viwango.
Aidha James amesema, uchunguzi umeanzishwa kwa miradi iliyobanika kuwa na kasoro na utakapokamilika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa.