Jumanne , 9th Feb , 2016

Msanii wa komedi bongo Mussa Yusuph maarufu kama ''Kitale'' amesema yeye ni brand hivyo huwa anahakikisha kila siku lazima ajiweke katika hali nzuri ya kimasoko ili watu mbalimbali waweze kumtafuta ili afanye nao kazi mbalimbali.

Kitale ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano katika kipindi cha Mkasi kinachorushwa na EATV, na kuongeza kuwa yeye kama msanii hua anajituma kwa hali na mali na kuweza kufanya vitu ambavyo vipo kila siku katika jamii lakini kwa lengo la kuchekesha watu.

''Mimi hua naigiza vitu hivi hivi ambavyo vinatokea katika jamii kila siku sema mimi nachukua na kuweka katika namna ambayo kila mtu akisikiliza au kutizama lazima acheke'' amesema Kitale

Aidha Kitale amewashauri wasanii wenzake wa kuigiza na kuchekesha kuhakikisha kuwa wanakuwa na mawazo tofauti kama wanavyofanya wanamuziki na sii kuigiza kitu kimoja kila siku na kwa aina moja ya muonekano jambo linalowafanya mashabiki kuwachoka.