Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miili ya watu 5 waliokufa maji Singida yapatikana

Jumatano , 7th Jul , 2021

Miili ya watu watano akiwemo mwanafunzi wa kidato cha nne waliokuwa wakihofiwa kufa maji Wilayani Singida imepatikana na kuopolewa baada ya juhudi za askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka mikoa mitano kushirikiana na wavuvi eneo hilo.

Picha mmoja ya mwili ulipoatikana baada ya juhudi za jeshi la la Zimamoto na Uokoaji ukiwa umezungukwa na wannachi

Watu hao watano waliokuwa wakisafiri na mtumbwi wa kienyeji kuelekea kwenye msiba kijiji cha Kinyento na kuzama Juni 5, mwaka huu majira ya asubuhi, walifariki baada ya mtumbwi ulikouwa ukiwavusha kuzama katika Bwawa la Ntambuka Kata Kinyeto.

Watu hao watano ambao wamepatikana wakiwa wamekwishafariki ni Ayubu Mohamed (39) Abubakar Hassani  (25) Abubakar Hamisi (35) Hamisi Ali (30) na  Ali Hamisi (18) ambaye ni mwanafunzi katika shule ya Sekondari Mrama Halmashauri ya wilaya Singida.

Taarifa za Jeshi la Zimamoto jana zilieleza kuwa katika mtumbwi huo walikuwemo watu saba ambapo wawili kati yao akiwepo nahodha waliokolewa na kukimbizwa hospitali kwa matibabu huku wakibakia watu watano ambao miili yao imepatikana jana kwa jitihada za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

Katika taarifa za awali zilizotolewa na Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (SACF) Ivo Ombella alisema chanzo cha ajali hiyo ni mtumbwi huo kupigwa na mawimbi makubwa katika bwawa hilo.

Kazi hiyo ya kuitafuta miili hiyo ilifanywa na Kikosi cha Jeshi la Zima Moto na Ukoaji kutoka mikoa ya Manyara, Singida Mwanza, Dodoma na Shinyanga kwa kushirikiana na wenzao wa Singida na wananchi.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali