Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Meya TEMEKE azungumzia kumng'oa Mtolea

Ijumaa , 23rd Aug , 2019

Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Chaulembo, amesema hana mpango wa kumng'oa Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea, kwa kuonesha nia ya kugombea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Meya Chaulembo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye kipindi cha East Africa Breakfast cha East Africa Radio, wakati akijibu swali juu ya mpango wake wa kugombea kiti cha Ubunge na kumng'oa Mbunge wa sasa wa jimbo la Temeke.

"Kuhusu mimi kutaka kuwa Mbunge, Watanzania wajue tunao wabunge wawili ambao ni Mtolea na Mangungu, mimi sijawahi kutamka kwamba nitagombea Ubunge, ila nimeonesha nia ya kwenda kugombea Usheikh wa Kata, na nimesikia fomu zimeshaanza kutoka nimwambie tu Sheikh wangu akae mkao wa kula, ila haya masuala ya Ubunge yanaletwa na Mungu." amesema Chaulembo.

Kuhusiana na Wilaya ya Temeke kuwa miongoni mwa Wilaya kinara kwa uchafu, Chaulembo amesema moja ya sababu ni Temeke kuwa na wakazi wengi.

"Unajua moja ya sababu Temeke kuongoza kwenye suala la uchafu, ikiwa tofauti na maeneo kama Arusha, Moshi au Iringa, usichokijua ni kwamba idadi ya wakazi wa Iringa ni sawa na Kata 1 Temeke, kingine Temeke lazima ujue ina mkusanyiko wa watu wa Mikoa mingi sana." amesema Chaulembo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali