Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbunge ampongeza Rais Samia kwa kunyanyua kilimo

Jumatano , 18th Mei , 2022

Mbunge wa Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameonesha kwa vitendo azma yake ya kuinyanyua sekta ya kilimo na wakulima ili izidi kutoa ajira kwa Watanzania wengi zaidi.

Mbunge wa Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma, Mariam Ditopile

Ditopile amesema kilimo ni muunganiko wa mambo mengi ikiwemo Utafititi na Utaalamu, Kilimo ni Sayansi, Teknolojia na Mitambo, Udongo, Mbegu, Maji kwa maana ya Maji na Umwagiliaji, Dawa na miundombini ya uvunaji na uhifadhi Pamoja na Soko hivyo kuishauri Serikali kuzingatia mtiririko huo ili kuleta tija kwenye kilimo.

"Kwa mara ya kwanza tumeshuhudia kwenye Nchi yetu hii ni bajeti ya kwanza inaletwa na Serikali na hakuna mtu analalamika kwamba ni ndogo hapa nimpe pongezi Rais Samia kwa hakika ameonesha yeye ni Mkulima mwenzetu na anajali kwa vitendo maslahi ya wakulima nchini na hilo amedhihirisha kwa kutuletea Waziri na Naibu Waziri wenye kujali wakulima.

Nitoe ushauri kwa Waziri na Naibu wake kuangalia watu wao wa chini haswa kwa maafisa wao ugani, Viongozi wa juu wanafanya kazi kubwa sana lakini hawa maafisa wao wa chini wanapaswa kufuatiliwa kwa karibu utendaji wao wasije kuangusha jitihada kubwa zinazofanywa na Rais Samia katika kuinua Kilimo.

Unaweza kuwa na Shamba lina ekari hata 1000 lakini usione hata Afisa Ugani anakuja kukutembelea, Tumeona Rais wetu amewapa vitendea kazi ikiwemo Pikipiki, Vipimia udongo ni wakati sasa wa Serikali kuwafuatilia maafisa hawa ili wasikae tu ofisini bali waende field kutoa elimu kwa wakulima," Mariam Ditopile.

"Niipongeze Serikali kwa kuongeza bajeti ya Kilimo hadi kufikia Sh Bilioni 751, tumeona mmehusisha vijana na niliwahi kushauri kuhusu hili kwamba vijana watengenezewe mazingira ya kushiriki kwenye kilimo na sasa tumeona kwa mipango mliyonayo kundi kubwa la vijana linakwenda kushiriki Kilimo.

Nishauri pia Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda na Biashara mkae pamoja mpange wote nini kinahitajika sokoni, Tuwe kama India Wizara ya Viwanda inatoa ushauri kwa Wizara ya Kilimo kwamba soko gani lipo ili wakashauri wakulima waje na zao ambalo liko sokoni hii itasaidia kukuza Soko la mazao yetu," Mariam Ditopile.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali