Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Matatizo ya wanafunzi wa bweni yatatuliwa

Jumapili , 18th Aug , 2019

Jumla ya wasichana 170 katika shule ya Sekondari Tura iliyopo Uyui Tabora,  wamepata taulo za kike watakazotumia kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Makabidhiano ya taulo za kike katika Shule ya Sekondari ya Tura

Shule hiyo iliyopo zaidi ya kilometa 150 kutoka Tabora mjini ni shule ya Bweni kwa wasichana ambapo Mkuu wa shule hiyo Adam Shaban Mangao, ameeleza kuwa taulo hizo zitasaidia kupunguza matatizo kwa wanafunzi wawapo bwenini.

''Kampeni ya Namthamini itatatua tatizo wanafunzi kubaki bwenini na kukosa masomo maana ndio tatizo ambalo limekuwa likisababisha kupunguza ufaulu kutokana na watoto hawa kulazimika kukosa vipindi wanapokuwa kwenye hedhi lakini hawajatumiwa fedha za kujikimu na kuweza kununua taulo hizi'', amesema.

Aidha Mwalimu Mangao, amezipongeza na kuzishukuru East Africa Television na East East Africa Radio kwa kuichagua shule ya Tura, kuwa miongoni mwa shule nyingi zitakazofikiwa na Kampeni ya Namthamini mwaka huu.

Zoezi la ugawaji wa taulo za kike katika shule 4 za mkoani Tabora lilikamilika Jumamosi Agosti 17, 2019, ambapo zaidi ya wanafunzi 500 wamepata taulo za kike kwa mwaka mzima.

Shule nyingine zilizofikiwa katika mkoa huo ni pamoja na Ikomwa, Ndono pamoja na Idete, ambapo timu ya East Africa Television na East Africa Radio iliambatana na mkuu wa mkoa huo Aggrey Mwanri.

Katika mwaka wake wa tatu, Namthamini imefanikiwa kufika katika mikoa ya Manyara, Arusha na Tabora huku ikitarajiwa kufika katika mikoa mingine ikiwemo Dodoma.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba