Kamanda Nyigesa amesema watu hao walikamatwa siku ya Agosti 13, katika Tarafa ya Yombo wilayani Bagamoyo mkoani humo wakiwa na orodha ya majina na namba za watu.
Inadaiwa majina na namba hizo walizokamatwa nazo zilikuwa ni kwa ajili ya kuwatapeli watu wapya na ambao wamekwishatapeliwa.
Pia watu hao walikutwa na simu 13 ndogo za tochi, Simu janja nne pamoja na laini 22 za
simu za makampuni mbalimbali.