Kw mujibu wa BBC inaonekana jaribio la mapinduzi linachukua hatamu kwa sasa. Milio ya risasi inasikika karibu na makazi ya Rais huku maeneo nyeti kama bunge, Televisheni ya Taifa na makazi ya Waziri mkuu yakizuiwa na magari ya kijeshi.
Inakumbukwa ni mwezi Januari mwaka huu ambapo kiongozi wa Taifa hilo kwa sasa Lt Col Paul-Henri Damiba, alipompindua Rais Roch Kaboré na kutwaa madaraka ya kijeshi.
Jana mamia ya waandamanaji waliingia mitaani huko magharibi mwa jiji la Bobo Dioulasso wakitaka kiongozi huyo wa kijeshi ajiuzulu wakimlaumu kwa ukosefu wa usalama nchini humo.
Mashuhuda wanasema kwamba wanaona vikosi vya kijeshi vikizunguka nchini humo , ambapo shule zimefungwa na wananchi wakisalia dnani kusubiria taaarifa za habari .