Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mapinduzi makubwa kwenye Afya na Elimu

Jumapili , 10th Oct , 2021

Waziri wa Fedha na Mipango Tanzania Dk. Mwigulu Nchemba ameweka wazi mpango wa matumizi ya fedha za mkopo wa Shilingi Trilioni 1.3 kutoka Shirika la Fedha Duniani (IMF) ambapo kwa kiasi kikubwa zitatumika kwenye miradi ya afya na elimu.

Waziri wa Fedha na Mipango Tanzania Dk. Mwigulu Nchemba

Dk. Nchemba amesema hayo leo Jumapili Oktoba 10, 2021 wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya Uviko-19 kwenye Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma.

''Kutokana na maelekezo yako Mhe. Rais, tunajenga madarasa elfu 15 kwa mpigo kwenye shule zetu za sekondari. Tunakwenda kujenga madarasa elfu 3 kwa mpigo kwenye shule za msingi. Tunaenda kununua madawati laki 462,795 ili kuondoa mbanano wa watoto,'' ameeleza Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha.

Kwa upande wa elimu ngazi ya vyuo Dk. Mwigulu amesema kuwa, ''Tunakwenda kumalizia shule za VETA katika mikoa 6 zilizopo kwenye hatuza za mwisho na 26 zilizokwama kwa muda mrefu. Tunajenga madarasa katika vyuo 17 vya ualimu na kuchapisha vitabu elfu 10,812 vya nukta nundu ili kuwaepusha wenzetu wenye matatizo ya kuona kuchangia vitabu''.

Kwenye upande wa afya Dk. Mwigulu ameeleza kuwa,''Mhe Rais tunakwenda kununua Digital X-Ray 85 kwa mpigo, pia tunakwenda kununua CT scan machine 29 kwa mpigo kwenye hospitali za mikoa yote ili watu wetu sasa wasihangaike kufuata huduma hii kwenye hospitali chache''.

Zaidi tazama video hapo chini
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali