Alhamisi , 10th Nov , 2016

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amewatembelea na kuwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli akimjulia hali Mke wake mama Janeth Magufuli aliyelazwa ktk Hospitali ya Muhimbili wodi ya Sewa Haji akipatiwa Matibabu

Miongoni mwa aliowatembelea ni Waziri na Balozi Mstaafu wa Tanzania Mhe. Omar Ramadhan Mapuri na Mkewe Mama Janeth Magufuli.

Rais Magufuli akimjulia hali Balozi Omari ramadhani Mapuri

Baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika wodi hiyo wamemshukuru Rais Magufuli kwa hatua zilizochukuliwa na Serikali kuboresha hospitali ya Taifa Muhimbili na wamebainisha kuwa licha ya kuboreshwa kwa mazingira ya hospitali pia wanap ata huduma nzuri kutoka kwa madaktari na wauguzi.