Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Madaktari mna''Stress'', - Waziri Jafo

Jumanne , 20th Aug , 2019

Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo amesema asilimia kubwa ya madaktari walioko nchini wana msongo wa mawazo kutokana na kazi kubwa ya kuhudumia watu waliyonayo.

Waziri Jafo ameyabainisha hayo leo Agosti 20 alipokuwa akizungumza na Waganga Wakuu wa Mikoa katika mkutano wao mkuu wa tatu uliofanyika mkoani Dodoma, ambapo amewapongeza kwa kazi yao kubwa, kwani wamekuwa wakijituma na kuwa mstari wa mbele kuokoa maisha ya watanzania.

''Niwapongeze madaktari wa Tanzania kwa kazi kubwa mnayoifanya, hili naomba nilisisitize nazungumza kwa dhati ya moyo wangu,  madaktari wetu mnafanya kazi kubwa sana ya dhati iliyopitiliza na mimi wakati wote nikiona mtu anabeza kazi ya madaktari huwa napata huzuni sana", amesema Jafo.

"Nimefika nilikuwa nawaangalia, wengi sana naona mna 'stress', mkutano umepooza,  ninachoamini kwamba wengi mnastress lakini stress hizo ni kwa kazi kubwa mnazofanya'' ameongeza Waziri Jafo.

Aidha katika pongezi zake  Waziri Jafo, ameeleza ni kwa namna gani aliwaona wakijitoa kuhudumia majeruhi wa ajali ya kulipuka kwa tenki la mafuta mkoani Morogoro.

''Mfano mzuri ni wa tukio kubwa la tenki la mafuta kuwaka moto Morogoro,nimefika pale mpaka saa tano za usiku, niliwaona madaktari hata mioyo
imeshakufa ganzi, watu waliokuwa katika hali mbaya, madaktari wakijituma kuwasindikiza Muhimbili
".

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali