Ijumaa , 4th Jul , 2025

Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo na waasi wa M23 wamesema kwamba watatuma wajumbe nchini Qatar kwa mazungumzo ya amani

M23 inashikilia eneo kubwa zaidi kuliko hapo awali mashariki mwa Congo baada ya kufanya harakati za mapema mwaka huu.

Mapigano hayo yamewaua maelfu ya watu na kuwafanya mamia kwa maelfu kuyahama makazi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mazungumzo hayo, waziri wa Mambo ya nje wa DRC Therese Kayikwamba Wagner amesema haya ni mazungumzo ambayo yalifanyika ndani ya mfumo wa mchakato wa Doha na ambayo lazima yaendelee ndani ya mfumo wa mchakato wa Doha. #EastAfricaTV