Akitoa sababu za kukwama kutolewa kwa uamuzi huo, Hakimu Chrisanta Chitanda, amesema anaiahirisha kesi hiyo hadi Machi 23 mwaka huu kutokana na hakimu anayesimamia kesi hiyo hayupo.
“Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Devotha Msofe, hayupo leo na hivyo naiahirisha hadi atakapokuwepo, Machi 23, mwaka huu,” amesema.
Awali ushahidi huo ulishindwa kuwasilishwa mahakamani hapo Januari 23 mwaka huu, baada ya upande wa utetezi kupinga kuwasilishwa mahakamani hapo sababu shahidi huyo siye aliyeandaa.