Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Lema aanika kinachomuumiza

Ijumaa , 17th Nov , 2017

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kupitia CHADEMA, ameweka wazi matatizo anayoyapata kama mbunge wa wananchi wake anaowatumikia, na kusema kwamba kama viongozi wao wanaumia zaidi wanapoona hawawaelewi wanachokifaya.

Lema ameyasema hayo kwenye mkutano wa hadhara akifanya kampeni kwa ajili ya chaguzi ndogo ndogo za udiwani katika kata ya Muriet mkoani Arusha, na kueleza kwamba wao kama wabunge wao wanajitoa muhanga kuwatetea wananchi wao, lakini huwa wanaumia zaidi pale wananchi hao kuonekana hawajali wala hawaoni jitihada zao.

Mimi ni mbunge ambaye nimekaa hospitali kumuuguza mbunge mwenzangu ambaye amepigwa risasi. Tundu Lissu amepigwa risasi kwa sababu ya kutetea uhuru wenu, tukiona hamuelewi mnatuumiza kuliko hao wanaotupiga, kama kuna kuna mateso tunapata kama viongozi wenu ni wakati nyie ambao tunawapigania hamtuelewi, tunaumia kuliko maelezo”, amesema Godbless Lema.

Godbless Lema ameendelea kwa kusema kwamba yeye binafsi anakumbana na changamoto nyingi kwani tangu apate wadhifa huo hajawahi kupata raha, kutokana na misuko suko anayoipata kutoka kwa jeshi la polisi na kudhalilishwa.

Toka nimekuwa mbunge wenu sijawahi kupata raha katika uongozi wangu, mimi ni mbunge ambaye nimepigwa sana, nimedhalilishwa sana na polisi, ni mbunge ambaye nyumbani kwangu polisi wamesachi mpaka nguo za ndani za mke wangu, kunidhalilisha na kutisha, nimekwenda jela miezi minne na siku 12, nimetekwa ili kuuawa, nimefukuzwa bungeni, kesi nilizonazo ni nyingi, nina kesi mbili dhidi ya Rais na siogopi, na haya yote kwa ajili yenu nyinyi”, amesema Godbless Lema.

Godbless Lema amekuwa mbunge ambaye mara kwa mara anakabiliana na jeshi la polisi kwa makosa mbali mbali anayotuhumiwa, ambapo mpaka sasa bado ana kesi zinazomkabili mahakamani.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali