Ijumaa , 12th Feb , 2016

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemteua tena mpinzani wake aliyekuwa muasi Riek Machar kuwa Makamu wa Rais wa taifa hilo changa la Afrika kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na televisheni ya taifa hilo.

Salva Kiir

Uteuzi huyo wa Machar uliotangazwa na televisheni ya taifa unachukuliwa kuwa ni sehemu ya makubaliano ya amani yanayolenga kumaliza machafuko yaliyodumu kwa muda wa miaka miwili.

Sudani Kusini imekuwa katika machafuko tangu Desemba 2013, wakati mapigano yalipoibuka baina ya vikosi vitiifu kwa Kiir na wanajeshi wanaomuunga mkono Riek Machar, ambaye awali alikuwa makamu wa Rais.

Riek Machar