Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kaimu Jaji Mkuu ataja atakaloanza nalo

Jumatano , 18th Jan , 2017

Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma ameahidi kumaliza kero ya ucheleweshwaji wa kesi kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika usajili na uendeshwaji wa kesi hizo.

Rais Magufuli akimuapisha Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Ikulu Dar es Salaam

Prof. Juma ametoa kauli hiyo mara baada ya kuapishwa na Rais Magufuli kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania katika  hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufaa na Mahakama ya Kuu na Viongozi wa Wizara ya Katiba na Sheria.

Jaji Prof. Ibrahim Juma amesema atakachoanza nacho ni kupitia sera mpya ya TEHAMA ili kuangalia jinsi ambavyo anaweza kuitumia katika kuiendesha mahakama kisasa zaidi zaidi.

Rais Magufuli katika picha ya pamoja na majaji wa mahakama ya rufaa

Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma amechukua nafasi ya Mhe.Jaji Mohamed Chande Othman ambaye amestaafu.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Hamis Juma alikuwa Jajiwa Mahakama ya Rufaa.

Rais Magufuli na baadhi ya watendaji wa mahakama

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao