Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kagera yatakata matokeo darasa la nne

Jumapili , 15th Jan , 2017

Mkoa wa Kagera umetakata katika matokeo ya mtihani wa upimaji wa kitaifa wa darasa la nne kwa kukamata nafasi ya kwanza kitaifa licha ya mkoa huo kukumbwa na janga la tetemeko la ardhi mwezi Septemba mwaka 2016.

Wanafunzi katika moja ya shule za msingi mkoani Kagera

Ufaulu katika mkoa huo ni asilimia 98.83 ambapo jumla ya wanafunzi 48,334 wamefaulu kati ya wanafunzi 48,907 waliofanya mtihani, ikifuatiwa na mikoa ya Kilimanjaro na Geita.

Katika matokeo ya mtihani huo uliofanyika mwezi Novemba mwaka jana (Miezi miwili baada ya tetemeko la ardhi) Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba pia ambayo pia iko ndani ya mkoa huo imeongoza katika halmashauri zote nchini.

Waliofaulu katika manispaa ya Bukoba ni wanafunzi 2,927 kati ya wanafunzi 2,936, ufaulu ukiwa ni asilimia 99.69 ikifuatiwa na Mji Makambako, na Tanga Mjini kama inavyoonekana katika majedwali yafuatayo.

Taarifa iliyotolewa leo na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kupitia kwa Katibu Mtendaji wake, Dkt. Charles Msonde, amesema jumla ya wanafunzi 950,167 kati ya wanafunzi 1,017,713 sawa na asilimia 93.36 waliofanya upimaji huo wameweza kupata alama zenye madaraja ya ufaulu wa A, B, C na D.

Amesema wanafunzi 67,547 sawa na asilimia 6.64 wamepata alama za daraja la E lenye ufaulu usioridhisha.

Takwimu za matokeo zinaonesha kuwa wanafunzi wamefanya vizuri zaidi katika somo la Stadi za Kazi, Haiba Na Michezo, ambapo asilimia 94.67 wamefaulu, huku wakifanya vibaya zaidi katika somo la English Language lenye ufaulu wa asilimia 72.51.

Katika wanafunzi 10 bora kitaifa, wanafunzi 8 ni wasichana wakiongozwa na Loi Martin Kitundu kutoka Fountain Of Joy, huku wanafunzi wawili pekee wakiwa ni wavulana.

Baraza hilo pia limeyafuta matokeo ya wanafunzi 58 waliobainika kufanya udanganyifu

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA