Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

JPM aweka makubaliano na Rais wa Afrika Kusini

Alhamisi , 15th Aug , 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, leo Agosti 15 amekutana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini Cyril Ramaphosa, Ikulu ya Dar es Salaam na kufanya mazungumzo ya faragha na kwa pamoja wameweka makubaliano yatakayoleta tija kiuchumi.

Katika hotuba yake Rais Magufuli amesema,  mazungumzo yake na mgeni wake yalijikita katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, ukizingatia nchi ya Afrika Kusini ni nchi yenye uchumi mkubwa barani afrika kwa kushika nafasi ya pili baada ya Nigeria, na kujadili namna ambavyo mataifa hayo yataweza kuimarisha biashara na uwekezaji.

''Tanzania na Afrika ya Kusini ni  washirika wakuu wa biashara tunaongoza kwa kuongoza kufanyabiashara ndani ya jumuiya ya nchi za SADC, Mwaka 2018 thamani ya biashara kati yetu  ilifikia dolla bilioni 1.8 kutoka dolla bilioni 1.1 mwaka  2017,  na sisi Tanzania  tuliuza Afrika Kusini bidhaa zenye thamani ya shilingi dolla milioni 743.02 ambayo ni sawa na asilimia 70 ya mazao yetu kwenye  nchi za SADC sawa na asilimia 16.7 ya mazao yetu yote nje ya nchi'', amesema Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli amewakaribisha wafanyabiashara wa Afrika ya Kusini, kuja kuwekeza nchini kwenye sekta mbalimbali ikiwemo kukuza sekta ya viwanda, afya , kilimo na uvuvi pamoja na usindikaji wa mazao mbalimbali.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali