Jumatatu , 4th Sep , 2017

Serikali mkoani Mara imezitaka kampuni binafsi kuwatumia walinzi waliopata mafunzo sahihi kutoka katika kambi mbalimbali za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) 

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Dkt. Charles Mlingwa, ambaye amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza vitendo vya ukosefu wa uaminifu kwa kampuni za ulinzi pamoja na kupunguza kuuawa kwa walinzi wasiokuwa na mafunzo yoyote.

Dkt. Mlingwa ameyasema hayo kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lidya Bupilipili katika hitimisho la mafunzo ya vijana zaidi ya 190 waliopitia mgambo  na  kupata mafunzo ya ulinzi kupitia  JKT Kikosi cha Rwamkoma 822 KJ.

Mkuu wa Kikosi hicho, Luteni Kanali David Msakulo amesema vijana hao wameiva kufanya kazi za ulinzi katika kampuni mbalimbali kwa uaminifu huku mkurugenzi wa Suma JKT, Meja Alfred Mwaijande akiwataka kuepuka vitendo vya Rushwa.