Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima
Dkt Gwajima ameongeza kuwa serikali pia imekua ikifanya nguvu kubwa ili kuhakikisha watu fulani wanaongoja maafa fulani kwa nchi yatokee bali yasitokee na kuomba wananchi ambao hawaitikii maelekezo waitikie ili hali iendelee kuwa salama zaidi.
"Watanzania wachukue tahadhari hali ingawa imedhibitiwa lakini inaendelea kuja na kasi ya wagonjwa kuendelea kujitokeza na kulazwa, watu wasidhani kwamba tunasubiri hali iwe basi mtaani tunaziona maiti ndiyo tuanze kazi, kazi inayofanyika ni kuifanya hali isiwe mbaya na serikali imekuwa ikijitahidi, wagonjwa wapo na wanaendelea kujitokeza na maambukizi yanaendelea kujitokeza na hii sio uongo,” amesema Dkt Gwajima.




