Ijumaa , 23rd Sep , 2022

umuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas)  imeamua kuiwekea vikwazo serikali ya kijeshi ya Guinea kutokana na kitendo chake cha kufanya mapinduzi ya kijeshi mwaka jana .

 Viongozi wa Jumuiya hiyo wamekutana huko New York ambapo wanahudhuria mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa. 

Wamekubaliana kuwawekea vikwazo idadi ya watu ambao idadi ya majina yao itatajwa muda wowote.  Viongozi wa kijeshi nchini  Guinea  wamesema kwamba wanahitaji miaka mitatu ili kuiweka nchi hiyo sawa kidemokrasia na kwamba hawaridhishwi na matakwa ya  Ecowas ya kutaka mabadiliko hayo yafanyike haraka iwezekanavyo. 

Guinea imeondolewa kwenye umoja wa Ecowas kufuatia mapinduzi ya kijeshi yaliyotokea  mwezi Septemba mwaka jana.