Alhamisi , 19th Jun , 2014

Kwa sababu zisizojulikana na wala bila taarifa yoyote kwa watumiaji wake, mtandano mkubwa duniani wa Facebook umetoweka hewani (facebook crushed).

Hali hiyo isiyotarajiwa na wengi, imetokea asubuhi hii ya kuanzia muda wa saa tano kasoro na kuwaacha watu wengi wanaotumia mtandao huo kujiuliza kinachoendelea.

Facebook huwa wana utaratibu wa kutoa taarifa kama kuna marekebisho watayafanya, ila kwa siku ya leo hakukuwa na taarifa yoyote, jambo linawatatiza watumiaji wake kitu kinachoendelea.