Jumatano , 23rd Oct , 2024

Jeshi la polisi mkoani mwanza limewakamata madereva wawili wa basi la Asante rabi Karim Auni (40) na Shedrack Swai (37) aliesababisha ajali iliyotokea octoba 22 jijini mwanza iliyoua watu 8 jijini na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Taarifa hiyo iliyotolewa na jeshi la polisi imeeleza jeshi la polisi linawashikilia madereva hao wa basi la kampuni hiyo kwa kuendesha basi kizembe na kusababisha ajali ambapo uchunguzi unaendelea na pindi uchunguzi utakapo kamilika watapandishwa mahakamani

Jeshi la polisi limeendelea kutoa wito kwa madereva wote wanaoendesha vyombo vya moto kuendesha kwa kuzingatia sheria na taratibu za usalama barabarani ili kuepusha ajali za mara kwa mara zinazoepikika.