Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

DC Pangani ataka watumishi wa siku nyingi watolewe

Alhamisi , 1st Jun , 2023

Mkuu wa wilaya ya Pangani, Zainabu Abdallah amekiomba Chama cha Mapinduzi mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na Wizara husika, kuwahamisha watumishi waliokaa muda mrefu katika wilaya hiyo ambao baadhi yao hawatekelezi majukumu yao na badala yake wamekuwa wakifanya kazi zao binafsi.

Mkuu wa wilaya ya Pangani, Zainabu Abdallah

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa sokoni ambao mgeni rasmi alikuwa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga Rajab Abrahamani  Abdalah (MNEC), mkuu huyo wilaya amesema kukaa kwao muda mrefu kumewafanya kutotimiza majukumu yao ipasavyo jambo linalokwamisha maendeleo wilayani humo. 

DC Zainabu amesema pamoja na jitihada nzuri za Rais, alikiri akiwa msimamizi wa shughuli za serikali Pangani kuna changamoto za baadhi ya watumishi hawatekelezi majukumu yao na badala yake wamekuwa wakifanya kazi zao binafsi ikiwemo kusimamia bodaboda na kusimamia masuala yao ya kifedha

"Mheshimiwa Mwenyekiti changamoto ya pili ni serikali kuwaleta watumishi walioharibu sehemu nyingine wanaletwa hapa Pangani siyo sehemu ya majaribio, tunataka watumishi wenye utayari wa kuwahudumia wananchi na kusikiliza kero zao, lakini siyo kuwa na watumishi wasiotekeleza wajibu wao," amesema DC Zainabu

Hata hivyo, alisema ,akiwa msimamizi mkuu wa shughuli za serikali hatafanya mzaha na mtumishi yeyote ambaye atakayerudisha nyuma maendeleo ya wananchi na alisema atampatia majina ya watumishi hao wanaoshindwa kwenda na kasi ya maendeleo ya wilaya hiyo kwa sasa.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti huyo wa CCM mkoa, alisema kuwa Pangani ile ya zamani siyo ya sasa, Pangani ya sasa inapiga hatua za maendeleo tangu mbunge Jumaa Aweso awe mbunge ambapo serikali imekuwa ikileta fedha nyingi za maendeleo.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali