Wakizungumza na #EastAfricaTV madereva wa Hiace wamedai kwamba bajaji zimekuwa zinaenda mpaka kwenye gari zao na kuwachukua abiria na kuwapeleka kwenye bajaji kwa kuwatoza shilingi 1000 wakati wao wanatoza nauli ya shilingi 600.
"Bajaji hazifuati utaratibu wa kuchukua abiria ndani ya kituo hiki Kwa kutufanyia vurugu na kuchukua abiria wetu,'' amesema Godfrey John na Hussein Ali ambao ni madereva wa Hiace
Baada ya mazungumzo kati ya bajaji, polisi na madereva wa hiace madereva bajaji walikubali kupisha kwenye hilo eneo walau ingawa wamedai kutoridhika kusogezwa kwenye kituo
Nao madereva wa bajaji wanaodaiwa kwenda kwenye hiace za Mbezi Msakuzi na kuchukua abiria wamesema kutokea kwa sintofahamu hiyo kumesababisha na madereva wa hiace kutaka waondolewe ndani ya kituo wakati wao waliwekwa kwa kuzingatia taratibu