
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga
Serikali ya Awamu ya Sita imeupatia mkoa wa Rukwa shilingi Bilioni Tatu na Milioni Mia Nane na Elfu Ishirini (3,820,000,000/-) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa katika halmashauri nne za mkoa wa Rukwa ambapo kila darasa litajengwa kwa shilingi Milioni Ishirini kupitia mfumo wa “Force Account”.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Sumbawanga Mhe. Sendiga amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wanafunzi wote wanapata mahala bora na salama kusomea.
“Natoa wito kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kufuatilia kwa ukaribu ujenzi wa madarasa hayo ili yaweze kukamilika kwa muda yaani ndani ya siku Sabini na Tano (75) kama alivyoelekeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI na kwa ubora ulioelekezwa pamoja na kukamilisha utengenezaji wa madawati yake” alisisitiza Sendiga.