
Mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa nchini Tanzania, Peter Kuga Mziray
Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha APPT Maendeleo, Peter Kuga Mziray, ameyasema hayo leo na kufafanua kuwa hatua hiyo inalenga kuzikutanisha pande mbili zinazokinzana ndani ya bunge maalumu la Katiba.
Mkutano huo utazikutanisha pande zote hasimu ndani ya bunge hilo na kuteua msuluhishi atakayewezesha mchakato wa Katiba mpya kuendelea baada ya kuwepo kwa maridhiano ya pande zote.