Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Aliyezuia polisi mahakamani ni wakili feki - TLS

Jumamosi , 27th Mei , 2023

Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimesema kuwa Baraka Mkama ambaye alitambulishwa kama wakili na kuonekana akiwazuia askari Polisi wasiwatie nguvuni  wateja wake baada ya kuachiwa huru na Mahakama sio wakili wala mwanachama wa TLS

Taarifa ya TLS imeeleza kuwa baada ya tukio hilo uongozi wa TLS uliunda kamati teule ya uchungzi wa tukio hilo na baada ya uchunguzi wamebaini mtu huyo sio wakili

Baada ya kupokea taarifa ya kamati, Baraza la Uongozi la TLS liliipitia na kuijadili, kwa hivyo, tunapenda kuwafahamisha Wanachama wote wa TLS, Wadau wa TLS na Umma wa Watanzania kwamba, TLS tumejiridhisha pasipo shaka kwamba mhusika wa tukio hilo ndugu Baraka Mkama sio wakili na sio mwanachama wa tanganyika law society.

Aidha TLS imeeleza kuwa  imepata taarifa muhimu za ziada kuhusu mtandao wa watu wasiokuwa mawakili wanaofanya kazi za uwakili (Vishoka) hivyo imeongezea muda Kamati Teule ya Uchunguzi kuendelea kufuatilia mtandao huo na kuwasilisha taarifa zake za ziada ifikapo tarehe 31 Mei 2023

Vilevile, TLS imekamilisha kuunda  kikosi kazi (Anti-Vishoka Taskforce) kitakachofanya kazi ya kudhibiti watu ambao hawastahili kufanya kazi za mawakili. Baraza la Uongozi la TLS linaomba ushirikiano toka kwa Wanachama wa TLS, Wadau wa TLS na Wananchi katika hizi juhudi za kutokomeza uhalifu huu. 

TLS inawakumbusha wananchi na wadau wake wote kila wakati kuhakiki taarifa za watu wanaoruhusiwa kufanya kazi za mawakili kwa kutumia mfumo wa utambuzi wa wakili wa Mahakama yaani e-wakili. TLS itahakikisha kuwa inalinda na kusimamia maslahi ya mawakili; itawalinda na kuwatetea wananchi dhidi ya vishoka; na kushirikiana na vyombo vya dola katika kudumisha hadhi, nidhamu na heshma ya Mawakili kama maafisa wa Mahakama wakati wote.
 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu