
Mwanamke huyo anadaiwa kufanya tukio hilo katika maeneo ya Tandika kwenye nyumba anayoishi ambapo Majirani walisikia sauti ya kichanga ikitoka kwenye nyumba hiyo na muda mchache hawakuisikia tena ndipo walipopata wasiwasi na kutoa taarifa Polisi
Chanzo cha tukio hilo ni baada ya mtuhumiwa kuona atazidiwa na majukumu ya kulea mtoto kwa kuwa alikuwa ana mtoto mwingine mdogo mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu ambaye bado ananyonya
Taarifa ya Polisi imesema kuwa uchunguzi wa awali umeonesha kuwa mtuhumiwa alijifungua salama na mtoto alikuwa hai lakini alikichukua kichanga hicho na kukiweka kwenye ndoo ndogo yenye ujazo wa lita kumi kisha kufunika ndoo kitendo kilichofanya akose hewa na kufariki #EastAfricaTV