
Mwenyekiti wa Halmashauri wilaya ya Ukerewe, Joshua Manumbu
Akiwa kwenye kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Joshua Manumbu, amesema kuwa watumishi waliofukuzwa kazi ni pamoja na aliyekuwa mtumishi wa maabara katika hospitali hiyo Baraka Bima, ambae alikiri mahakamani kuhusika na wizi wa dawa hizo na mtendaji wa kijiji cha Bukonyo Sabato Mashauri, aliyepatikana na kosa la kuomba rushwa kiasi cha shilingi laki moja na elfu hamsini.